HII KALI: MWILI WA MKUU WA KUNDI LA WAUZA ‘UNGA’ MEXICO ALIYEUAWA WAIBIWA.
Katika
hali isiyokuwa ya kawaida maiti ya mmoja wa viongozi wa mtandao wa
madawa ya kulevya waliokuwa wakitafutwa sana nchini Mexico Heriberto
Lazcano aliyeuawa umeibiwa kutoka katika nyumba yalikokuwa yakifanyikia
mazishi yake.
Rais
wa Mexico Felipe Calderon amelipongeza jeshi kwa operesheni
iliyofanikisha kuuawa kwa Lazcano, aliyekuwa mkuu wa kundi la Zetas
ambalo limefanya mauaji ya kikatili, katika vita dhidi ya madawa ya
kulevya nchini Mexico.
Takriban
watu elfu 60 wameshauawa katika mgogoro kati ya makundi mbali mbali ya
madawa ya kulevya na polisi tangu Rais Calderon aingie madarakani mwaka
2006.
No comments:
Post a Comment